ABIRIA Treni ya Shirika la Reli la Tanzania na Zambia (TAZARA )waliotoka Mkoani Mbeya stesheni ya Iyunga tangu Septemba 17,2021 Wamekwama katika stesheni ya TAZARA Makambako Mkoani Njombe huku wakidai kupata changamoto mbalimbali ikiwemo ya kushinda njaa kutokana na kuishiwa fedha.
Akizungumza mjini Makambako, abiria Bw.Rubeni Simchimba ,amesema alikata tiketi yeye na watoto wake watatu ambao anawapeleka chuo Ifakara Mkoani Morogoro tangu Septemba 17 mwaka huu 2021 saa 3 asubuhi na ilipofika jioni wakataarifiwa kuwa warudi makwao hadi watakapojulishwa.
"Mwandishi wa habari Mimi nilishtushwa na kauli hiyo natokea Mkoani Songwe Wilaya ya Momba mawasiliano yangu na wenzangu watayapataje ? Amehoji Bw.Simchimba.
Juhudi za kuwanusuru abiria hao hazikuzaa matunda kutokana na Afisa aliyepatikana wa Makao makuu ya TAZARA Dar es salaam kutokuwa tayari kuzungumzia suala hilo kwa njia ya simu. Hata hivyo juhudi zinafanyika kuwasiliana na Wizara ya Uchukuzi ili kuona namna nzuri itakayofaa kuwasaidia abiria hao.





0 Comments