Mwanamke mmoja Mkazi wa mtaa wa
Mtwivila B ,Manispaa ya Iringa aliyefahamika kwa jina la Rehema
Ismail amekutwa amefariki na mwili wake ukiwa umetelekezwa kando ya barabara inayounganisha mitaa ya Mtwivila B
na Mtwivila C mkoani Iringa.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Mtendaji wa kata ya
Mtwivila Thadei Mhanga, amesema alipokea taarifa ya tukio hilo mnamo majira ya saa mbili asubuhi leo oktoba 29,2021.
Jeshi la polisi Manispaa ya Iringa limefika katika eneo la tukio na kuchukua mwili kwaajili ya uchunguzi zaidi.
0 Comments