AJALI YAUA WAWILI NA WENGINE KUJERUHIWA


Watu wawili wamefariki dunia na wengine 25 kujeruhiwa baada ya basi la kampuni ya SEA kugongana  na lori katika kijiji cha Unyenye Wilayani Mlele Mkoa wa Katavi.

Kwa mujibu wa mashuhuda  wamesema ajali hiyo imesababishwa na mwendokasi na uzembe wa dereva wa basi ambaye alikuwa akifukuzana na madereva wenzake wa mabasi mengine mawili yaliyokuwa katika msafara mmoja yakitokea  katika stendi ya Majimoto mkoani humo.

Akithibitisha  kutokea kwa ajali hiyo Kamanda  wa polisi mkoa wa Katavi Benjamini Kuzaga amesema taarifa zaidi zitatolewa kuhusu ajali hiyo  huku mganga mkuu wa Halmashauri ya Mpimbwe ,Martine Lohay akithibitisha kupokea majeruhi 25 na miili miwili ya watu waliofariki kutokana na ajali hiyo.

Post a Comment

0 Comments