KILICHOCHELEWESHA MAZISHI YA HAMZA HIKI HAPA


Mwili wa Hamza Mohamed ambaye alifariki dunia katika majibizano ya risasi kati yake na polisi hatimae umezikwa  katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es salaam majira ya saa 2:30 usiku .

Kwa mujibu wa msemaji wa familia ya Hamza ,Abdulrahm Hassan amesema Mazishi yalitarajiwa kufanyika mchana saa saba lakini haikuwa hivyo kwa sababu ya kazi ya kutoa risasi zilizokwama .

Mwili huyo ulizikwa baada ya kuswaliwa katika msikiti wa Mamuur uliopo Upanga jijini Dar es salaam.

Post a Comment

0 Comments