Mwili wa Hamza Mohamed ambaye alifariki dunia katika majibizano ya risasi kati yake na polisi hatimae umezikwa katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es salaam majira ya saa 2:30 usiku .
Kwa mujibu wa msemaji wa familia ya Hamza ,Abdulrahm Hassan amesema Mazishi yalitarajiwa kufanyika mchana saa saba lakini haikuwa hivyo kwa sababu ya kazi ya kutoa risasi zilizokwama .
Mwili huyo ulizikwa baada ya kuswaliwa katika msikiti wa Mamuur uliopo Upanga jijini Dar es salaam.
0 Comments