SIMBA QUEENS YAAGA CECAFA

Timu ya Wanawake ya Simba, Simba Queens safari yake imehitimishwa hii leo baada ya kupokea kipigo cha 2-1 dhidi ya Vihiga Queens katika mchezo wa nusu fainali.

Kipigo hicho walichokipata Simba Queens kinahitimisha safari yao katika Mashindano ya CAF Women’s Champions League CECAFA Qualifiers kwa mwaka huu 2021.

Mchezo huo ulipigwa katika dimba la Nyayo stadium na kuwaacha Simba Queens wakishuhudia Vihiga Queens wakitinga hatua ya fainali ya michuano hiyo.

Post a Comment

0 Comments