Baraza la Mitihani Tanzania (Necta) limewafutia matokeo watahiniwa 393 waliobainika kufanya udanganyifu katika mitihani ya kuhitimu darasa la saba 2021.

Katibu Mtendaji wa Necta, Dk Charles Msonde amesema baraza limezishauri mamlaka husika kuwachukulia hatua wote waliohusika na udanganyifu huo.

“ Baraza limezishauri mamlaka kuwachukulia hatua wale wote waliohusika kwa namna moja au nyingine kusababisha kutokea  kwa udanganyifu katika mitihani”  Dk Msonde.

Msonde amesema pia baraza limezuia kutoa matokeo ya watahiniwa 128 ambao waliugua au kupata matatizo na kushindwa kufanya mtihani kwa masomo yote au baadhi ya masomo

Watahiniwa hao wamepewa fursa nyingine ya kufanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi kwa mujibu wa kifungu 32(1) cha kanuni za mitihani.

 Kupata matokeo: BONYEZA HAPA KUANGALIA