Fiston Mayele

Klabu ya yanga itawakosa nyota watatu wa kimataifa Kuelekea mchezo wa CAF champions league dhidi ya Rivers Unitedwaliosajiliwa msimu huu kutokana na kuchelewa kwa hati za uhamisho kutoka kwenye vilabu vyao vya zamani.

Khalid Aucho

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam msemaji wa klabu hiyo Haji Manara amewataja wachezaji hao watakaokosekana kuwa ni Djuma Shaban ,Khalid Aucho na Fiston Mayele .

Djuma Shaban

Aidha amewataka mashabiki na wanachama wa klabu hiyo kuwa wavumilivu kwa kipindi hiki wanachosubiri taarifa kamili kutoka TFF ya idadi ya mashabiki watakaoruhusiwa kushuhudia mchezo huo uwanjani