CAF wanataka kocha mkuu awe na leseni ya UEFA A PRO ambayo ni sawa na CAF A.
Thierry ni mmoja wa walimu wanaoheshimika Rwanda na aliwahi kuwa msaidizi wa Didier Gomez wakati Rayon Sports ikitwaa ubingwa wa ligi kuu nchini humo.
Mrwanda huyo ni msomi wa shahada ya Uzamili katika masuala ya Fedha aliopata nchini Ubelgiji pia ana leseni ya ukocha daraja A inayotolewa na CAF.
Simba ambayo inatetea ubingwa wa ligi msimu huu imejipanga pia kufanya vizuri kimataifa baada ya msimu uliopita kutupwa nje na Kaizer Chiefs ya Afrika kusini kwa mabao 4-3 katika hatua ya robo fainali ya ligi ya Mabingwa Afrika.
0 Comments